Nuru FM

DC Kheri ahimiza kuongeza nguvu katika malezi ya watoto

27 May 2024, 10:33 am

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kheri James akizungumzia kuhusu usawa katika malezi ya watoto. Picha na Adelphina Kutika

Wazazi wameshauriwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao na kujenga mahusiano mazuri ya kirafiki na ya ukaribu ili kuwaweka karibu watoto na kuwafanya wawajue wazazi wao vizuri.

Na Adelphina Kutika

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kheri James amewahimiza wananchi kuhakikisha wanaunganisha nguvu katika malezi ya watoto wote katika jamii  zinawazunguka ili kulinda ustawi wao na kutimiza   ndoto zao.

DC Kheri ameyasema hayo katika hafla ya kukabidhi vyakula katika familia (49) vilivyotolewa  na Kituo cha (FISCH) Future For Iringa Children  Manispaa ya Iringa wakati akizungumza  na wananchi , watoto na viongozi wa kituo cha FISCH .

Sauti ya DC Iringa

Awali akiwasilisha taarifa mbele ya mgeni rasim Mnufaika wa kituo cha FISCH na Mkurugenzi Wa kituo cha FISCH Alexanda Joseph Magelanga amesema wana jumla ya wanafunzi wapatao 34 ambao wanapata elimu ya vyuo vikuu na vyuo vya kati ikiwemo ufundi.

Sauti ya Mkurugenzi Fisch

Kwa upande wao baadhi ya wazazi waliofika katika hafla hiyo Joyce Rashidi Mkonjela na Elizabeth Kisoma  wamekishukuru kituo hicho kwa kuwahudumia watoto wao  na kupata fursa ya kupata elimu ili kutimiza ndoto zao kutokana na mazingira magumu walionayo wazazi hao.

Sauti ya Wazazi

Yusuphu Emmy Longole  ni mmoja wa watoto wanaonufaika na kituo cha fisch  ameeleza namna anavyosaidiwa ili kutimiza ndoto zake.

Sauti ya Watoto

MWISHO