Nuru FM

Shirika la SOS kuweka usawa malezi na makuzi ya Mtoto Iringa

24 May 2024, 1:49 pm

Viongozi wa Shirika la SOS wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Halmashauri Mafinga Mji. Picha na Joyce Buganda

Malezi na makuzi Bora kwa mtoto imetajwa kuwa sababu inayopelekea kuongeza kujiamini kwa watoto Mkoani Iringa

Na Joyce Buganda

Shirika la SOS children’s villagers wamefanya kikao cha kujadili na kushawishi ongezeko la bajeti katika shuhuli za ulinzi wa mtoto huku lengo kubwa likiwa kuweka usawa katika malezi na  makuzi ya  watoto.

Akizungumza katika kikao kilichowajumuisha madiwani wa halmashauri ya mafinga mji,  na idara ya ustawi wa jamii wa halmashauri hiyo  Meneja Mradi wa shirika la SOS children’s  villagers  Mkoa wa  Iringa Bw. Victor Mwaipungu   amesema shirika la SOS  lilianza mda mrefu na mpaka sasa lipo katika nchi 135 duniani kote na kwa Mkoa wa Iringa shirika hilo lilianza mwaka 2016 kwa mwaka huo lilianza na mradi wa elimu.

Sauti ya Meneja SOS

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa jamii wa halmashauri ya Mafinga mji  Stella Mbeye amesema kwa upande wa Mafinga mji walijitahidi kuifikia jamii kwa kufanya vipindi vya redio zaidi ya 8,  kufanya mikutano na wazazi, kwenda mashuleni kutoa elimu  kujumuika katika maadhimisho mbalimbali kama siku 16 za kupinga ukatili na siku ya mtoto wa afya kwa upande wa watoto

Sauti ya Ustawi

Peter Ngusa ni Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Mafinga mji amesema suala la kuongeza bajeti  kwa  ulinzi na usalama wa watoto ni la muhimu lakini pia watakaa na madiwani katika vikao vyao ili kujadili suala hilo  ili kulipeleka mbele zaidi Taifa la watoto.

Sauti ya Ngusa

MWISHO