Mpanda FM

Recent posts

6 April 2023, 9:18 am

Kamati ya PETS Yabaini Madudu Shule za Msingi Nsimbo

NSIMBO Kamati ya ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za umma katika shule za msingi (PETS) halmashauri ya Nsimbo imebaini uwepo wa uchakavu wa miundombinu,ukosefu wa vyoo mashuleni na uhaba wa walimu. Akisoma taarifa ya Awali wakati akiwasilisha taarifa ya Mrejesho…

6 April 2023, 8:46 am

Serikali Kutatua Mgogoro wa Kagera Group Dhidi ya Wanakijiji Dirifu

MPANDA Serikali imehaidi kutatua mgogoro uliopo kati ya bodi ya kagera group na wanakijiji wa dirifu kata ya magamba ,manispaa ya mpanda mkoani katavi. Hayo yamesemwa na katibu tawala wa manispaa ya Mpanda Kenneth Pesambili akimwakilisha mkuu wa wilaya ya…

6 April 2023, 8:36 am

Kamati ya Shule za Msingi Imetakiwa Kufatilia Miradi Katika Shule za Msingi

MPANDA Kamati za shule za msingi katika halmashuri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi zimetakiwa kuhakikisha zinafuatilia miradi inayofanyika katika shule za msingi. Hayo yamezungumzwa na kaimu afsa elimu msingi wa halmashuri ya manispaa ya Mpanda Victor Mwakajumlwa katika semina…

4 April 2023, 5:55 am

Wananchi Makongolo Walia na Ukosefu wa Maji

MPANDA Wananchi wa kijiji cha Makongolo kata ya magamba halamshauri ya manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wameulalamikia uongozi wa kijiji hicho kwa kushindwa kutatua changamoto ya maji ambayo imekuwa kikwazo katika shughuli zao za kila siku. Wakizungumza na kituo hiki…

4 April 2023, 5:53 am

Wananchi Mpanda Watoa Maoni Mseto Juu ya Damuchafu

MPANDA Baadhi Ya wananchi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wametoa maoni mseto juu ya wimbi lililoibuka la watu wanaofanya matukio ya kupora na kuiba mitaani maarufu kama Damu Chafu. Wameyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati wakizungumza na kituo hiki…

4 April 2023, 5:51 am

Mtoto wa Siku 14 Atelekezwa Mlangoni

KATAVI Mtoto mchanga anayekadiriwa kuwa na umri wa siku 14 amekutwa ametupwa kwenye mlango wa nyumba ya Jenifa Donald mkazi wa Tambukareli mtaa wa Shauritanga Manispaa ya Mpanda. Mashuhuda wa tukio hilo wakizungumza na Mpanda radio wamebainisha kuwa mtoto huyo…

4 April 2023, 5:49 am

Wananchi Kayenze Walia Ucheleweshwaji wa Mradi wa Maji

KATAVI Wananchi wa Kayenze kata ya Katuma Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi wameiomba serikali kumhimiza mkandarasi anayejenga mradi wa maji kukamilisha mradi kwa wakati. Wananchi Kwa nyakati Tofauti wameiambia Mpanda radio kuwa kumekuwa na adha kubwa ya upatikanaji wa maji safi…

31 March 2023, 1:31 pm

Mikopo ya Asilimia 10 Yaendelea Kutolewa Nsimbo

NSIMBO Wanawake,vijana na watu wenye ulemavu kutoka katika halmashauli ya nsimbo mkoani Katavi wameendelea kunufaika na mikopo ya 10% ambayo inatolewa katika halmashauri hiyo. Akisoma taarifa ya utowaji wamikopo afisa maendeleo kutoka katika halmashauli ya nsimbo Lucy Kagine amesema kuwa…

30 March 2023, 3:38 pm

Wananchi Tanganyika Waomba Elimu ya Afya ya Meno na Kinywa

KATAVI Baadhi ya wananchi wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi wameomba kupatiwa elimu ya afya ya kinywa na meno kabla ya kupata athari. Wakizungumza na Mpanda radio Fm wamekiri kupata huduma bora ya afya ya meno huku wakiomba serikali kutoa elimu…

Kuhusu Mpanda Radio

Umiliki wa redio
Mpanda Radio FM inamilikiwa na kampuni iliyosajiliwa iitwayo Mpanda radio FM Limited na cheti cha usajili namba 78298 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpanda Radio FM pia imesajiliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania TCRA, Wizara ya Viwanda na biashara; ama tunatambuliwa na Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania TCCIA na Mamlaka ya Mapato ya Tanzania kama Mlipa Ushuru, tuna Namba ya Kitambulisho cha Mlipa kodi 115-577-239 na tumepewa nambari ya usajili ya VAT 40-015708 kwa Biashara iliyoko hoteli ya Mpanda, eneo la eneo. nambari G, nambari ya kuzuia 35.

Dira
Kuwa jamii thabiti yenye afya bora, elimu, umoja na maendeleo endelevu, inayotambua wajibu na haki.

Dhamira
Kushirikisha jamii katika kuandaa vipindi, habari na uendeshaji wa redio kwa kuzingatia taaluma. Kuwa jukwaa la mijadala inayochochea mabadiliko chanya ya fikra, usawa wa jinsia, sheria na utawala bora, uwajibikaji, ushindani wa maendeleo, utamaduni na ulinzi wa rasilimali.

Uongozi
Mpanda Radio FM ina mlolongo mzuri wa uongozi na inasimamiwa na Bodi ya wakurugenzi. Tuna wakurugenzi watatu kwa hisa na kuajiriwa; pia tuna uongozi wa uzalishaji na uuzaji.