Nuru FM

Villa aombwa kutatua changamoto ya Maji na barabara

9 April 2026, 09:03

Wananchi wa Jimbo la Mafinga wakiwa katika mkutano wa Mbunge wa Jimbo lao Mh. Dickson Lutevele VILLA. Picha na Fredrick Siwale

Changamoto ya Maji na Barabara imetajwa kukwamisha shughuli za kimaendeleo kwa wananchi wa jimbo la Mafinga.

Na Fredrick Siwale

Wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini Mkoani Iringa wameiomba serikali kutatua changamoto ya Maji na Ubovu wa miundombinu ya barabara.

Wakizungumza katika Mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, Mh. Dickson Lutevele VILLA, wananchi hao wamesema kuwa katika eneo la Lumwago kuna changamoto ya Barabara sambamba na changamoto ya Maji katika Mtaa wa Mkombwe.

Sauti ya Wananchi
Mbunge Villa akizungumza na wananchi wa Jimbo lake

Naye Diwani wa Kata ya Boma Mh. Baraka Kisakanike amesema kuwa Kata ya Boma imekuwa na changamoto ya ubovu wa barabara hasa katika kipindi hiki cha Mvua.

Sauti ya Diwani

Akijibia changamoto hizo, mbunge wa Jimbo la Maafinga Mjini Mh. Dickson Lutevele VILLA amesema kuwa kuna mradi wa maji unatekelezwa  utakaotoa lita Milion 11 kwa siku.

Sauti ya Mbunge

Kuhusu changamoto ya Barabara Mh. Villa amesema kuwa watashirikiana na Tarula na kuanza kufanya ukarabati wa barabara korofi mara baada ya mvua kupungua. MWISHO