Nuru FM

Asas akemea makundi ndani ya CCM

10 February 2026, 3:42 pm

MCC Salim Asas akizungumza kwenye kikao Cha Halmashauri Kuu CCM Wilaya ya Mufindi. Picha na Fredrick Siwale

“Makundi ndio sababu ya kushindwa kuleta maendeleo kwa jamii, Tuyavunje tuwe wamoja”

Na Fredrick Siwale

Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa wametakiwa kuvunja makundi waliyo kuwanayo wakati wa uchaguzi ili waweze kuwatumikia wananchi.

Hayo yamezungumzwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa MCC  Salim Asas walipokuwa mgeni wa katika kikao Maalumu Cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Mufindi na kuongeza Kuwa makundi hayana faida Kwa Sasa na badala yake waungane kwa pamoja kutatua changamoto za wananchi.

Sauti ya Asas

“Yake makundi yaliyijitokeza wakati wa uchaguzi mkuu, na sasa ni muda wa kuvunja makundi yote Kwa sababu Tumehimizwa kuachana nayo, na haya makundi yakiendekezwa chama kitavunjika na lazina tuondoe majereha ya majina ya watu kukatwa” Alisema Asas

Awali Mwenyekiti wa wa CCM Wilaya ya Mufindi George Kavenuke amesema Kuwa wameshafanya vikao na Mikutano katika maeneo yote ya Wilaya ili kurudisha Ari ya utendaji kazi kuanzia ngazi ya shina na majimbo yote.

Sauti ya Kavenuke

Naye Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mh. David Kihenzile amemshukuru Mjumbe wa Kamati Kuu Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa MCC  Salim Asas kwa kusimamia vyema uchaguzi uliotamatika bila yeyote kujiusisha na rushwa.

Sauti ya Kihenzile