Nuru FM

Mhapa awa Mwenyekiti wa Halmashauri Iringa DC

4 December 2025, 2:49 pm

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Steve Mhapa akizungumza katika Baraza la Madiwani. Picha na Joyce Buganda

“Tushirikiane katika kuwatumikia wananchi ili kuleta maendeleo”

Na Joyce Buganda

Diwani wa kata ya Nzihi Steven Mhapa amefanikiwa kutetea Nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa halmashauri  ya wilaya ya Iringa kwa kura 37 kati ya kura 37 zilizopigwa huku kiti cha makamu  mwenyekiti wa halmashauri hiyo kikienda kwa  Mheshimiwa  Constantino Makala.

Akizungumza mara baada ya uchaguzi huo ambao uliambata na kikao cha kwanza cha baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mheshimiwa Steven Mhapa ameushukuru uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Iringa kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kuongoza halmashauri hiyo kwa kipindi cha miaka mitano kama mwenyekiti  huku akisisistiza umoja na mshikamano uliokuwepo uendelee.

Sauti ya Mhapa

Anord Mvamba ni katibu itikadi na uenezi wa halmashauri ya wilaya ya Iringa amempongeza mheshimiwa Mhapa kwa kuchaguliwa kwa kishindo  na kusema ushindi huo unaonyesha  ameamininwa na madiwani wenzie pamoja na wananchi wa wilaya hiyo.

Sauti ya Mvamba

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mahuninga  Michael Vahaye amesema ndani ya siku 100 za kwanza atajitahidi kushirikiana na wataalamu wa halmashauri  na mbunge wake katika kusimamia na kumalizia miradi iliyokuwa haijamalizika.

Sauti ya Diwani

Baraza hilo  la kwanza kwa Halmaushauri ya Wilaya ya Iringa lilifanyika katika ukumbi wa  makao makuu ya halmashauri hiyo uliopo ihemi  ambapo sambamba na uapisho kwa madiwani na uchaguzi wa mwenyekiti na makamu wa halmashauri baraza hili lilijadili kamati mbalimbali kama mpango kazi wa mwaka 2025mpaka 2030.