Nuru FM

Iringa yapokea magari 9 ya zimamoto

21 October 2025, 11:07 am

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James Akiwa katika Uzinduzi wa magari ya zimamoto Iringa. Picha na Ayoub Sanga

“Magari haya yatasaidia kupunguza majanga ya moto katika jamii” RC Kheri

Na Hafidh Ally

Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Kheri James amekabidhi rasmi magari na vitendea kazi vya kisasa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kuimarisha utendaji wa Jeshi hilo katika kukabiliana na majanga mbalimbali yanayoweza kutokea katika jamii.

Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa hivyo Komred Kheri James ameeleza kuwa lengo la kukabidhi vifaa hivyo ni kuwa na majeshi imara yenye askari wenye nidhamu, utiii na vifaa vinavyo weza kutoa huduma bora kwa raia na mali zao.

Sauti ya RC Kheri

Aidha RC amebainisha kuwa Mkoa wa Iringa umepokea magari tisa yenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za aina yoyote inayotokea katika jamii, na vifaa vya kisasa vya kurahisisha uokoaji na kulinda usalama wa waokoaji.

Sauti ya RC Kheri

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Iringa, Jackline Mtei, amesema ujio wa magari hayo utasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza ufanisi wa jeshi hilo katika kushughulikia matukio ya moto na uokoaji ndani ya mkoa.

Sauti ya Mtei

Nao wananchi Manispaa ya Iringa wameishukuru serikali kwa kulwezesha jeshi hilo kupata magari hayo ambayo yatasaidia kukabiliana na matukio ya moto katika jamii.

Sauti ya Wananchi