Nuru FM

Machinga Complex Iringa kuwa suluhu ya wajasiriamali

14 October 2025, 9:48 am

Mgombea wa Ubunge Jimbo la Iringa Mjini Fadhili Ngajilo akiwa na wanachama wa CCM katika Mikutano ya Kampeni. Picha Adelphina Kutika

Kukamilika kwa ujenzi wa Soko la Machinga Complex Iringa utarasihisha wajasiriamali kufanya kazi zao kwa uhuru.

Na Adelphina Kutika

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Fadhili Ngajilo, amesema kukamilika kwa ujenzi wa Soko la Machinga Complex kutakuwa suluhisho la changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara wadogo katika Manispaa ya Iringa.

Akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni Uliofanyika  kata ya Ilala, Ngajilo amesema mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipita mkoani Iringa kuomba kura na kuahidi kukamilisha ujenzi wa soko hilo, ambalo sasa linatarajiwa kuwa mkombozi mkubwa kwa wamachinga.

Sauti ya Ngajilo

Aidha Ngajilo, ameahidi kushirikiana kwa karibu na Serikali kuhakikisha kero zinazowakabili wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Iringa (Frelimo) na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa zinapatiwa suluhisho la kudumu ili wananchi wapate matibabu bora, yenye staha na kwa wakati.

Sauti ya Ngajilo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Iringa Mjini, Isack Kikoti, amewataka vijana wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi na kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Sauti ya Kikoti