Nuru FM

Mvamba: Vijana shirikini kwenye Uchaguzi 2025

24 September 2025, 9:49 am

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iringa Vijijini, Ndugu Arnold Mvamba akiwanadi wagombea wa Chama Chao. Picha na Ayoub Sanga.

“Vijana ndio hazina ya Leo hivyo wanapaswa kuchagua viongozi wanaowataka kwa maslahi Yao na Taifa” Alisema Mvamba

Na Hafidh Ally

Vijana Wilaya ya Iringa wameaswa kutokukubali kuathiriwa na taarifa za kupotosha zinazozagaa kwenye mitandao ya kijamii kwa lengo la kuwavunja moyo na kuwazuia kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za uchaguzi katika Kata ya Lumuli, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iringa Vijijini, Ndugu Arnold Mvamba, amesema baadhi ya watu wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kusambaza taarifa zenye kuleta , taharuki , hofu na propaganda zinazolenga kuwakatisha tamaa wananchi hasa vijana, ili wasijitokeze kupiga kura ifikapo Oktoba 29, 2025.

Sauti ya Mvamba

Aidha amewataka kuchagua viongozi bora kwa kuwa kesho iliyobora inajengwa leo kwa kuchagua kiongozi mwenye kiu ya kuleta maendeleo.

Sauti ya Mvamba

Kwa upande wake Mgombea Udiwani wa CCM Kata ya Lumuli, Ndugu Abeid Kisinini amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi kimeweza kuleta maendeleo hivyo ni wakati wa wananchi kuendelea kuwaamini kwani serikali imeboresha huduma za shule na Miundombinu ya Barabara.

Sauti ya Mgombea

Naye Mgombea wa Ubunge Jimbo La Kalenga Jackson Kiswaga amesema kuwa serikali imeendelea kufanya shughuli za kimaendeleo ikiwemo kusambaza umeme ambapo ni muda sasa wa wananchi kuwapa kura ya ndio katika uchaguzi mkuu ili wazidi kuwapatia maendeleo.

Sauti ya Kiswaga