Nuru FM

Polisi Iringa watoa tamko wizi wa mifugo

17 May 2024, 8:54 am

ACP Allan Bukumbi akizungumzia mikakati wa kukomesha wizi wa mifugo Mkoani Iringa. Picha na Joyce Buganda

Wizi wa mifugo umekuwa desturi iliyoenea na wakati mwingine inayosababisha wafugaji kuwa maskini jambo lililopelekea jamii hiyo kuazimia namna ya kukabiliana na changamoto.

Na Joyce Buganda

Wizi wa mifugo watajwa kuwa kikwazo kikubwa kwa wadau wa ufugaji mkoani iringa  huku wafugaji wakitakiwa  kuwa na ushirikiano na jeshi la polisi ili kukomesha yabia hiyo.

Akizungumza kwenye kikao cha wafugaji na jeshi la polisi kamishna msaidizi, mwandamizi  wa jeshi la polisi na Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa ACP Allan Bukumbi amesema ili kukomesha tabia hiyo inatakiwa kila mfugaji afanye utafiti wa mifugo.

Sauti ya ACP Bukumbi

Naye Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa iringa Riziki Makwaya amesema kwa kipindi cha Januari mpaka Aprili  kwa mwaka huu ni matukio 14 ya uhalifu yameripotiwa hivyo matukio yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Sauti ya Makwaya

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Wilaya ya Iringa Emanuel Sairuti amesema wataendelea kutoa ushirikiano na jeshi la polisi ili kutokomeza  na kumaliza kabisa.

Sauti ya Mwenyekiti wa wafugaji

MWISHO