Nuru FM

Asas: Vijana tumieni mitandao kuyasemea mazuri ya Rais

1 October 2024, 9:57 am

Salim Asas akizungumza na Vijana wa CCM Iringa. Picha na Adelphina Kutika

Na Adelphina Kutika

Vijana wa Uvccm mkoa wa Iringa wametakiwa  kutumia  mitandao ya kijamii  kuzungumza mazuri yanayofanywa serikali na serikali ya awamu ya sita.

Agizo hilo limetolewa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Asas,wakati akifunga mafunzo  ya siku saba kwa vijana wa UVCCM mkoa wa Iringa yaliyofanyika katika chuo cha Vijana cha Ihemi na kuhimiza kuwa Vijana wajikite kuelezea mafanikio ya serikali na sio kupiga picha zisizofaa.

Sauti ya ASAS

Kwa upande wake Katibu wa UVCCM Mkoa wa Iringa, Aisha Mpuya, amesema vijana waliopata mafunzo hayo ni 370 kwa lengo la kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa, kuelewa mafanikio ya serikali ya awamu ya sita lakini pia kujifunza matumizi bora ya mitandao.

Sauti ya Aisha

Mjumbe wa kamati ya utekelezaji UVCCM wilaya Mufindi Jamsini  Ng’umbi amesema semina hiyo imewajenga vijana kuwa wazalendo wa kukisemea vizuri chama na taifa kwa ujumla

Sauti ya Jasmini

MWISHO