Nuru FM

Polisi Iringa yawatunuku vyeti wakaguzi na askari

14 March 2025, 12:11 pm

Kamanda Allan Bukumbi akikabidhi cheti kwa askari mkoani Iringa. Picha na Adelphina Kutika

Na Adelphina Kutika

Jeshi la polisi mkoa wa Iringa  limewapongeza  wakaguzi  na askari  waliofanya vizuri   mwaka 2024  ili kuongeza chachu  kwa wengine kufanya kazi kwa nidhamu na weledi

Akizumgumza katika hafla hiyo ya kukabidhi vyeti hivyo  kamanda wa polisi mkoa wa iringa ACP Allan Bukumbi katika viwanja  vya FFU Kihesa amesema  lengo la kutoa  motisha na kuthamini utendaji kazi kwa askari hao na  kuongeza morali katika utekelzaji wa majukumu.

Sauti ya Kamanda

Awali akiawasilisha taarifa fupi mbele ya Mgeni Rasim mkuu wa kitengo operation na Mafunzo mkoa wa  Iringa  meloy Buzema amesema hafla hiyo ya kutambua utendaji kazi kama mkoa wameona achache waliofanya kazi vizuri  wakaguzi 2 na askari 6.

Sauti ya Mkuu

Kwa upande  wao waliotunukiwa  vyeti vya sifa ya pongezi  akiwemo Mkaguzi Msaidizi kata kata ya Mkwawa Feruzi Makamba amepongeza  uongozi  wa jeshi la polisi  kwa kutambua  mchango wao na kuahidi  kuendelea kufanya kazi  kwa kuzingatia  kwa weledi.

Sauti ya Askari

Hata hivyo huo ni utaratibu wa  wa kawaida kwa jeshi la polisi   mkoa wa  Iringa  kutambua  na kutambua na kuwa pongeza  askarin  na wakaguzi waliofanya vizuri  ili kuhamasisha  utndaji kazi kujenga taswira  chanya ka jamii.

MWISHO