FM Manyara

Shirika la So They Can  Tanzania  (STC) laratibu kambi ya matibabu Babati

15 September 2026, 1:55 pm

Picha ya Wananchi wa kata ya gallapo wakihudumiwa katika kambi ya matibabu inayofanyika katika shule ya msingi OIM

Kambi ya Matibabu ya afya inayoratibiwa na Shirika la So They Can  Tanzania  (STC) imeanza rasmi sept 14 katika shule ya msingi OIM iliyopo kata ya Galapo Wilayani Babati mkoani Manyara  ambayo itafanyika kwa siku sita.

Na Marino Kawishe

Akizungumzia huduma zitakazotolewa kwenye kambi  hiyo Meneja wa  shirika la STC Tanzania Roselyne Mariki amesema huduma zitolewazo ni pamoja na uchunguzi wa Saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake, Huduma za uchunguzi wa macho  pamoja na vipimo vingine ikiwemo kinywa na Meno na uchunguzi wa afya ya akili na ushauri na sahaa.

 

Meneja wa  shirika la STC Tanzania Roselyne Mariki

Naye Mratibu wa kambi hiyo ya Afya na Muuguzi mkuu kutoka Hospital ya Halmashauri ya Wilaya ya Babati Sister  Thea Funto amewataka wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Halmashauri hiyo hasa kwenye kata zitakazofikiwa na kambi hiyo kujitokeza kwa wingi kupata matibabu ambayo yanaratibiwa Bure na Shirika hilo.

Muuguzi mkuu kutoka hospital ya halmashauri ya Wilaya ya Babati

Kambi hiyo ya afya iliyoanza  sept 14 imefadhiliwa na shirika la So They Can Tanzania, KCCO, Kafika House, FreeO2, Sibusiso na Chuo cha ualimu maalumu  Patandi na  itaendelea tena kwa siku tano katika kata za Galapo, Qash, Endakiso na Mamire zilizopo Wilayani Babati mkoani Manyara. 

Mwananchi akipatiwa huduma ya Vipimo vya Macho katika kambi ya matibabu Gallapo