FM Manyara

Naibu Waziri Regina Ndege achangia mifuko 100 ya saruji kujenga daraja Mamire

27 July 2026, 8:04 pm

Picha ya Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara, Regina Ndege

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara, Regina Ndege ametoa mifuko 100 ya saruji na kuahidi kutembelea daraja lililokatika kwa mvua zilizopita na  linalounganisha kitongoji cha Waloa na Kijiji cha Mwikantsi katika kata ya Mamire Wilayani Babati Mkoani Manyara

Na Marino Kawishe

Akizungumza na Waamini wa Parokia ya Mt Karol Langwa Mamire kwenye jubilee  ya miaka 25 ya kwaya  hiyo Naibu waziri  amesema atatembelea kuona athari zilizosababishwa na mvua zilizopita ambazo ziliharibu kivuko cha eneo hilo.

Sauti ya Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara,

Aidha kwa upande wake Diwani wa kata ya Mamire Augustino Sosiya akimkaribisha Naibu waziri amegusia Umuhimu wa kivuko hicho na kuomba kiweze kufanyiwa matengezo ya haraka kabla ya mvua kuanza kunyesha tena ambapo kijiji Tayari kimetenga kiasi cha sh milion 5.

Sauti ya Diwani wa kata ya Mamire