FM Manyara
FM Manyara
20 May 2026, 5:38 pm

Leo ikiwa ni kilele cha siku ya vipimo duniani, wananchi mkoani Manyara wametakiwa kufahamu vipimo sahihi wanaponunua bidhaa za mchanga, mawe kokoto na pumba ili kuepuka kununua bidhaa hizo zikiwa na ujazo usio sahihi.
Na Mzidalfa Zaid
Wito huo umetolewa na meneja wakala wa vipimo mkoa wa Manyara Denis Misango wakati akiongea na fm Manyara amesema wamekuwa wakifanya ukaguzi kwa kupima malori yanayobeba bidhaa hizo na kufahamu yamebeba ujazo kiasi gani.
Amesema ili mwananchi afahamu kama lori limehakikiwa lazima liwe na stika kutoka wakala wa vipimo ambayo inakuwa inaonyesha ujazo wa bodi, ambapo amewaonya baadhi ya madereva wasio waaminifu ambao wamekuwa wakiwadanganya wananchi kwa kuandika ujazo usio sahihi kwenye gari tofauti na ujazo ulizojazwa katikagari hilo.