FM Manyara

Jamii Manyara yatakiwa kupinga usafirishaji haramu wa binadamu

13 August 2026, 4:52 pm

Picha ya Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu Makao Makuu Dodoma, Consolatha Tarimo

Jamii mkoani Manyara imetakiwa kutoa taarifa kwa mamlaka husika inapobaini vitendo vya usafirishaji haramu wa binadamu, ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa na Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu Makao Makuu Dodoma, Consolatha Tarimo, wakati akitoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kutambua na kupinga vitendo hivyo kupitia kipindi Cha mseto wa Leo kinachorushwa Fm Manyara radio.

Sauti ya Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu Makao Makuu Dodoma, Consolatha Tarimo

Tarimo amesema ushirikiano wa wananchi ni muhimu katika kukabiliana na usafirishaji haramu wa binadamu, pamoja na kuhakikisha waathirika wanapata msaada na ulinzi unaostahili.