FM Manyara

Wafungwa watakiwa kufuata sheria kutumia kifungo cha nje

14 July 2026, 10:32 pm

Picha ya Afisa huduma za uangalizi mwandamizi Mkoa wa Manyara,Tumain Mosha

Wafungwa waliopatiwa adhabu ya kifungo kisichozidi miaka minne wametakiwa kufuatilia  haki yao ya kuomba kutumikia sehemu ya kifungo  chao wakiwa nje kupitia huduma kwa jamii, endapo watatimiza vigezo na masharti yaliyowekwa kisheria.

Na Mzdalfa Zaid

Hayo yameelezwa na Afisa huduma za uangalizi mwandamizi Mkoa wa Manyara,Tumain Mosha, amesema huduma kwa jamii ni mfumo wa utekelezaji wa adhabu unaolenga kuwapa nafasi wafungwa wanaostahili kutumikia kifungo chao wakiwa katika jamii chini ya uangalizi badala ya kuendelea kukaa gerezani kwa kipindi chote cha kifungo.

Sauti ya Afisa huduma za uangalizi mwandamizi Mkoa wa Manyara,Tumain Mosha

Aidha, amesema moja ya sifa muhimu ni  mfungwa awe amehukumiwa kifungo kisichozidi miaka minne, na akisisitiza  kuwa  kila maombi hufanyiwa tathmini  kwa kuzingatia masharti ya sheria ya huduma  kwa jamii kabla ya uamuzi  kufanyika.