FM Manyara
FM Manyara
3 March 2026, 9:10 pm

Halmashauri ya wilaya ya Babati imefanya kongamano la Wanawake katika shule ya msingi Vilima vitatu lenye lengo la kujadiliana kuhusu masuala ya haki za wanawake na wasichana kuelekea siku ya wanawake.
Na Marino Kawishe
Akizungumza baada yakukamilika kwa kongamano hilo afisa maendeleo halmashauri ya wilaya ya Babati January Bikubwa amesema mada zote zilizopangwa zimejadiliwa kikamilifu.
Aidha Mwakilishi wa shirika la STC Tanzania Grace Swai ambaye amezungumzia Maada inayolenga wanawake na dira ya Taifa ifikapo 2050 amesema lazima malezi kwa vijana ni jambo lakuangaliwa na jamii yote ili kufikia malengo ya Dira hiyo.

Naye mwanasheria kutoka Shirika la CSP Eliakim Warikoy akitoa maada kwenye Kongamano hilo amesema kuwa jamii inapaswa kuacha kuendeleza mila potofu ambazo zimekuwa kichocheo cha ukatili kwenywe baadhi ya maeneo hapa Mkoani Manyara.

Maadhimisho ya siku ya wanawake kiwilaya yanatarajiwa kufanyika March 6 mwaka huu katika uwanja wa mpira wa kijiji cha Nkaiti Katika kata ya Nkaiti kuanzia asubuhi hadi jioni.