FM Manyara

Serikali Manyara yasitisha mnada wa mali za umma zilizotangazwa kuuzwa

17 April 2026, 8:24 pm

picha ya baadhi ya mali zilizokuwa zimeandaliwa kwa ajili ya kupigwa mnada

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara kupitia katibu Tawala msaidizi rasilimali Dominic Mbwete,  amesitisha mnada wa mali za umma zilizokuwa zimetangazwa kuuzwa katika  mnada kutokana na kuibuka sintofahamu kutoka kwa wafanyabiashara waliohudhuria kwa ajili ya  kununua mali hizo.

Na Mzidalfa Zaid

Akiongea baada ya wafanyabiashara hao kulalamika, Mbwete amesema wameamua kusitisha mnada huo hadi April 18 2026 ili changamoto hiyo kutatuliwa na kutolewa tamko rasmi.

sauti ya katibu Tawala msaidizi rasilimali Dominic Mbwete,
picha ya baadhi ya mali za umma

Kwa upande wao wafanyabiashara ambao wametoka maeneo tofauti hapa nchini wamesema mnada ulikuwa unafanyika kwa kinyume na taratibu ambapo wameishukuru serikali ya mkoa wa manyara kwa kuingilia kati mgogoro huo.

sauti ya wafanyabiashara wakilalamika