FM Manyara
FM Manyara
7 August 2026, 6:20 pm

Mamlaka ya Bonde la Maji Pangani Kanda ya Kaskazini, inayohudumia mikoa yaArusha na Kilimanjaro, imetoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo, pamoja na umuhimu wa kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji.
Na Emmy Peter
Elimu hiyo imetolewa katika Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Temi njiro, mkoani Arusha.
Akizungumza katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bonde laMaji Pangani Segule Segule, amesema taasisi hiyo ina jukumu la kusimamia na kuhifadhi rasilimali za maji, ili kuhakikisha zinatumika kwa uendelevu kwa manufaa ya wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Maabara, Nikolaus Germanus, amesema Mamlaka hiyo hutoa pia huduma za upimaji wa ubora wa maji kwa wakulima, hususan maji yanayotumika katika shughuli za umwagiliaji.
Amesema upimaji huo huwasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi kuhusu matumizi ya maji, pamoja na kuhakikisha maji wanayotumia yana ubora unaofaa kwa shughuli za kilimo, hatua inayochangia kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao.