FM Manyara

Bonde la Pangani latoa elimu ya uhifadhi wa vyanzo vya maji

7 August 2026, 6:20 pm

Picha ya pamoja ya watumishi wa Bodi ya maji Bonde la Pangani

Mamlaka ya Bonde la Maji Pangani Kanda ya Kaskazini, inayohudumia mikoa yaArusha na Kilimanjaro, imetoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo, pamoja na umuhimu wa kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji.

Na Emmy Peter

Elimu hiyo imetolewa katika Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Temi njiro, mkoani Arusha.

Akizungumza katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bonde laMaji Pangani Segule Segule, amesema taasisi hiyo ina jukumu la kusimamia na kuhifadhi rasilimali za maji, ili kuhakikisha zinatumika kwa uendelevu kwa manufaa ya wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Sauti ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bonde laMaji Pangani Segule Segule,

Kwa upande wake, Mkuu wa Maabara, Nikolaus Germanus, amesema Mamlaka hiyo hutoa pia huduma za upimaji wa ubora wa maji kwa wakulima, hususan maji yanayotumika katika shughuli za umwagiliaji.

Sauti ya Mkuu wa Maabara, Nikolaus Germanus

Amesema upimaji huo huwasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi kuhusu matumizi ya maji, pamoja na kuhakikisha maji wanayotumia yana ubora unaofaa kwa shughuli za kilimo, hatua inayochangia kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao.