FM Manyara
FM Manyara
10 August 2026, 11:51 am

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Kanda ya Kaskazini EWURA imewataka wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji kwakufungua vituo vya mafuta huku mamlaka hiyo ikiwahakikishia kuwa mamlaka inasimamia utoaji wa vibali na leseni za ujenzi na uendeshaji kwa kuzingatia sheria na viwango vya usalama.
Na Marino Kawishe
Akizungumza na Fm Manyara kutoka viwanja vya Nane nane Njiro Jijini Arusha Meneja wa EWURA Kanda ya Kaskazini George Mhina amesema ili kuanzisha au kuwekeza kwenye kituo cha mafuta nchini Tanzania kunahitaji kufuata hatua na masharti yaliyowekwa na mamlaka husika.
Aidha amesema masharti hayo ni pamoja na umiliki wa eneo likiwa na Hati miliki au kibali halali cha matumizi ya ardhi kwa eneo linalokusudiwa, pamoja na Tathimini ya Mazingira ambapo utakuwa nanyaraka ya cheti cha mazingira kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na usimamizi wa mazingira (NEMC).
