FM Manyara
FM Manyara
10 October 2024, 5:04 pm

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura zoezi ambalo litaaanza October 11 hadi October 20 mwaka huu.
Na Mzidalfa Zaid
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Manyara kimewataka wananchi wenye sifa na nia ya kugombea nafasi za uongozi wa Serikali za Mitaa kujitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa.
Akiongea na wanahabari kwenye ofisi za chama hicho, Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) Mkoa wa Manyara Peter Toima amesema chama hakitaangalia mtu au kazi hivyo kila mtu ana haki ya kugombea.
Katika hatua nyingine Toima amewataka wananchi mkoani Manyara kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ili washiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.
Aidha, amesema chama hicho hakitakwenda na viongozi wasiofaa ambao walioshindwa kutekeleza majukumu yao katika kipindi kilichopita nakusema wanaataka viongozi watakaotekeleza ilani za chama cha mapinduzi