FM Manyara
FM Manyara
13 August 2026, 5:15 pm

Taasisi ya Chem Chem imekabidhi darasa Moja lililofanyiwa Maboresho,mashine ya kudurufu na computer mpakato mbili kwa Uongozi wa Shule ya Msingi Mdori iliyopo katika Kata Ya Nkaiti Wilayani Babati mkoani Manyara.
Na Marino Kawishe
Akisoma taarifa ya mradi huo wa miaka minne kwa mgeni Rasmi katibu Tawala wilaya ya Babati Tobias Abwao, Mkuu wa Shule ya msingi Mdori John Bura amesema mradi huo umegharimu zaidi ya shilingi milion 23 ambapo utakuwa kila mwaka unatengeneza Darasa Moja mpaka kumalizika kwake.
Aidha Mgeni Rasmi kwenye Halfa hiyo katibu tawala wilaya ya Babati Thobias Abwao Ameutaka uongozi wa shule kulinda rasilimali hizo walizopewa na Taasisi ya Chem Chem ili zitume kwa lengo lilikusudiwa.
Kwa upande wake afisa mradi ya jamii kutoka Chem Chem Napendael Wazoel Amesema Lengo lao nikuisaidia Jamii kupitia uhifadhi ambao umeendelea kuwanufaisha Wananchi ambao wapo pembezoni mwa hifadhi na ushirikiano wao ndio umepelekea wawekezaji kufanya kazi bila kikwazo.
Mradi huo utanufaisha wanafunzi 460 wanaosoma kwenye shule hiyo na utakamilika 2029.
