FM Manyara
FM Manyara
24 April 2026, 1:02 pm

Mfuko wa Taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF) mkoa wa Manyara imewashauri wananchi kujiunga na kuchangia (NSSF) kwa wale ambao wamejiajiri au sekta binafsi kupitia mfuko hifadhi skimu yaani mpango maalum unaolenga kuwawezesha wananchi walioajiriwa kujiunga na kuchangai (NSSF) kulingana na kipato chao.
Na Mzidalfa Zaid
Ushauri huo umetolewa leo na Meneja wa mfuko wa Taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF) Alexanda Joseph, wakati akiongea na fm Manyara, amesema mpango huo unawapa fursa wananchi waliojiajiri kujiunga na kuchangia (NSSF) kulingana na kipato chao.
Amesema faida za kujiunga ni pamoja na kupata sehemu ya akiba kwa dharura, kuchukua michango yake endapo atasitisha uanachama, kupata fao la matibabu, uzazi pamoja na msaada wa mazishi.
Aidha, amesema walengwa wa skimu hiyo ni pamoja na, wakulima, wafugaji, wavuvi, wachimbaji wadogo, wasanii,machinga, bodaboda,wafanyabiashara wadogo na makundi yote ya waliojiajiri.