FM Manyara

Ubadilishaji wa mita za kisasa za umeme unaendelea

23 June 2026, 10:29 pm

Picha ya mita janja (Smart Meter)

Zoezi la ubadilishaji wa mita za kisasa za umeme  (Smart Meter) linaendelea katika Mkoa wa Manyara na sasa limeingia katika  awamu ya pili  ambapo linafanyika katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Manyara  kwa lengo la kuboresha huduma za umeme na kuongeza  ufanisi katika usimamizi wa matumizi ya nishati.
 
 Na Mwandishi wetu
 
Akizungumza na fm Manyara  afisa uhusiani wa shirika la umemee Tanesco mkoa wa Manyara  Samuel Mandari ,amesema wananchi wameendelea kujitokeza na kutoa ushirikiano kwa mafundi wanaotekeleza zoezi hilo, huku  wakieleza matarajio yao ya kupata huduma bora zaidi kupitia matumizi ya mita hizo za kisasa.

Sauti ya Afisa uhusiani wa shirika la umemee Tanesco mkoa wa Manyara

Aidha Mandari amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana  na shirika hilo wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo ili kuhakikisha linafanyika kwa mafanikio na kukamilika kwa wakati .