FM Manyara

Vituo vya taarifa na maarifa vyatoa tathmini ya mradi kwa vikundi 56 Manyara

29 April 2026, 1:13 am

Picha ya wanavikundi kutoka kwenye vituo vya taarifa na maarifa katika kata ya Mamire na Murray wakiwa katika Warsha

Na Marino Kawishe.

Jumla ya wanavikundi 56 kutoka kwenye vituo vya taarifa na maarifa katika kata ya Mamire na Murray Mkoani Manyara wametoa tathimini ya utekelezaji mradi uletao mabadiliko ambao unatekelezwa kwenye halmashauri 6 na mikoa mitatu hapa nchini.

Wakizungumza na Fm Manyara Radio Wawakilishi wa vikundi hivyo wamesema zipo changamoto kadhaa ambazo zimekwamisha kufikia lengo la mradi huo na moja wapo ikiwa ni elimu.

Sauti ya Wawakilishi wa vikundi
Picha ya Msimamizi wa mradi kutoka mtandao wa Jinsia Tanzania Catherine Kasimbazi

Kwa Upande wake Msimamizi wa mradi huo kutoka mtandao wa Jinsia Tanzania Catherine Kasimbazi amesema lengo la kuanzishwa kwa mradi huo ni kutambua na  kuwawezesha kuinuka kiuchumi  wakulima ambao wanafanya kazi na mtandao huo wa Jinsia hapa Tanzania  

Sauti ya Msimamizi wa mradi kutoka mtandao wa Jinsia Tanzania

Warsha hiyo ya siku mbili imeanza April 28 na  imehudhuriwa na maafisa mbali mbali wa serikali kutoka ngazi ya kijiji hadi halmashauri zilipo kata hizo.

Picha ya wanavikundi kutoka kwenye vituo vya taarifa na maarifa katika kata ya Mamire na Murray wakiwa katika Warsha ya kufanya tathmini