FM Manyara

Kampuni ya PASS Leasing Limited yanufaisha wakulima nane nane Arusha.

5 August 2026, 11:25 pm

Picha ya Mkuu wa Wilaya ya Rombo Raymond Mwangwala pamoja na viongozi wa Kampuni ya PASS Leasing Limited wakimkabidhi Mkulima Trekta.

Kampuni ya PASS Leasing Limited inayotoa mikopo ya vifaa vya kilimo Imekabidhi Trekta aina Holland kwa mkulima kutoka Wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro lenye  Thamani ya zaidi ya shilingi milion 70.

Na Marino Kawishe

Akikabidhi Trekta Hilo Mkuu wa Wilaya ya Rombo Raymond Mwangwala amesema Kampuni hiyo imeendelea kuwa  msaada kwa wakulima mbali mbali  Hapa Nchini na Kutekeleza kikamilifu sera ya Rais Samia Suluhu Hasan kwenye Dira ya Taifa 2050.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Rombo

Kwa upande wake Mkulima huyo amesema Kupata Trekta hilo litamuwezesha kufanya shughuli za kilimo kikamilifu na kuishukuru Kampuni ya PASSLeasing kwa kuendelea kuwawezesha Wakulima.

Sauti ya mkulima

Aidha Afisa Mkuu wa PASS Leasing Kanda ya Kaskazini Neema  Nyangalamela  amesema wakulima waendelee kuwaamini Kampuni hiyo kwani Mikopo ya kilimo bado ipo hata baada ya Maonesho ya 32 ya nane nane mwaka 2026.

Sauti ya Afisa Mkuu wa PASS Leasing Kanda ya Kaskazini

Maonesho hayo yanaongozwa na kauli mbiu inayosema kuwa  ” Tambua Soko : Ongeza Tija  kutekeleza Dira 2050.