FM Manyara

MATI Super Brand yapongezwa kuongeza ajira kwa vijana

1 May 2026, 7:39 pm

picha ya Mkurugenzi wa kampuni ya MATI David Mulokozi  

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga, ameipongeza Kampuni ya MATI Super Brand ya mjini Babati mkoani Manyara kwa kuwaajiri vijana wengi na kupunguza changamoto ya vijana kuwa tegemezi .

Na Mzidalfa Zaid

Sendiga amesema hayo leo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ambayo yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, amesema amefuarahishwa na uwekezaji huo na kuwataka wawekezaji wengine kuiga mfano huo.

sauti ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Kwa upade wake Mkurugenzi wa kampuni ya MATI David Mulokozi  amesema kampuni ya mati wameadhimishwa siku hii kwa kishindo huku akielezea  dhamira yake ya kukuza uchumi wa Tanzania kupitia sekta ya viwanda, utalii na hifadhi za mazingira.

sauti ya Mkurugenzi wa kampuni ya MATI David Mulokozi

Aidha, katika maonyesho hayo, Kampuni ya MATI Super Brand imejinyakulia kombe pamoja na zawadi mbalimbali ikiwemo banda bora na maandamano bora.

baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya MATI SUPER BRAND