FM Manyara
FM Manyara
24 June 2026, 1:01 am

Wafugaji na wanunuzi wa kuku Wilayani Babati mkoani Manyara wamelishukuru Shirika la Hand in Hand kwa kuwakutanisha pamoja kujadili juu ya mahusiano ufugaji na soko la kuku.
Na Christina Christian
Wakizungumza kwenye jukwaa la mahusiano ya kibiashara kwa wadau katika soko la kuku lililofanyika wilayani Babati wamesema jukwaa hili linakwenda kuwafungulia fursa mbalimbali za kibiashara kwani wamekutana limewaunganisha pamoja kibiashara.
Wamesema Shirika la Hand in Hand limekuwa msaada mkubwa kwao kwani wanafuga kisasa na kuwarahisishia katika masoko na mnunuzi kupata kuku bora kutoka moja kwa moja kwa mfugaji
kwa upande wake Meneja wa Shirika la Hand in Hand tawi la Manyara Yona Onna amesema kuwa lengo la jukwaa hili ni kuwakutanisha pamoja ili kuweza kujenga na kufahamu changamoto wanazokutananazo ili kuzitafutia ufumbuzi
