FM Manyara
FM Manyara
25 April 2026, 11:50 am

Mkoa wa Manyara umeaadhimisha miaka 62 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo upandaji wa miti , kufanya usafi katika halmashauri ya mji wa babati pamoja na kufanya michezo mbalimbali.
Na Mzidalfa Zaid
Akiongea kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga,mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda, amewataka wananchi kuendelea kuimarisha amani na mshikamano.
Amesema Taifa la Tanzania limeendelea kuwa mfano wa utulivu wa kisiasa,mshikamano wa kijamii , na maendeleo ya kijamii ambapo yote hayo yamesababishwa na umoja uliwekwa na mwalimu julias nyerere na shekhe amani karume.
Kwa upande wake katibu tawala mkoa wa Manyara Mariam Muhaj, amesema katika kuadhimisha siku hiyo wamepanda miti katika maeneo mbalimbali ya mkoa , kufanya usafi pamoja na mazoezi.

Nao baadhi ya wazee kutoka mkoani Manyara ambao walishuhudia muungano huo mwaka 1964, wamesema wamefurahia uwepo wa muungano kutokana na umoja na amani iliyopo.
Maadhimisho ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar huadhimishwa april 26 kila mwaka, na kwa mkoa wa Manyara maadhimisho hayo yameadhimishwa leo na kauli mbiu ya miaka 62 ya muungano kwa mwaka huu ni amani, umoja na mshikamano ni msingi wa maendeleo endelevu.


