FM Manyara
FM Manyara
19 May 2026, 4:56 pm

Wananchi mkoani Manyara, wametakiwa kuchukua tahadhari ya ugonjwa Ebola unaosababishwa na virusi vya Ebola kutokana na ugonjwa huo kuwa miongoni mwa magonjwa ya milipuko, kufuatia ugonjwa huo kuwa tishio katika baadhi ya nchi za afrika mashariki ikiwemo nchi ya Uganda na Congo.
Na Mzidalfa Zaid
Wito huo umetolewa na mratibu wa huduma za tiba mkoa wa Manyara Elford Mukerebe wakati akiongea na fm Manyara, amesema daliliza za ugonjwa huo ni pamoja na homa kali ya ghafla, kulegea kwa mwili, maumivu ya misuli, kuumwa kichwa, vidonda kooni, kutapika, kuhara , vipele kwenye ngozi, na kutokwa damu sehemu za wazi .
Kwa upande wake afisa afya mkoa wa manyara Suten Mwabulambo,amewataka wananchi kuepuka kugusa maiti ya mtu aliyekufa kwa dalili za ugonjwa huo,kuepuka kutumia nguo, na vyombo vilivyotumiwa na mtu mwenye dalili hizo na akiwahimiza wananchi kuzingatia usafi kwa kunawa mikono kwa maji safi na salama.