FM Manyara

 Yas Tanzania yapeleka huduma za mawasiliano Gendabi

22 May 2026, 7:44 pm

Picha ya mnara mpya wa mawasiliano Kampuni ya Yas Tanzania wenye uwezo wa 4G

Kampuni ya simu za mikononi ya Yas na Mixx by Yas  Tanzania wamezindua mnara wa mawasiliano wenye uwezo wa 4G plus kwenye kijiji cha Gendabi Wilayani Hanang Mkoani Manyara. 

Na Marino Kawishe

Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho Kiongozi wa Kanda ya Kaskazini kutoka mtandao huo Robert Sanyagi  amesema lengo la Kampuni ya Yas na Mixx by Yas  Tanzania nikufikisha huduma bora za mtandao kwa jamii na hasa maeneo ambayo yanachangamoto kubwa  za mawasiliano.

sauti ya Kiongozi wa Yas Kanda ya Kaskazini Robert Sanyagi 
picha ya Kiongozi wa Kanda ya Kaskazini kutoka mtandao huo Robert Sanyagi  akizungumza na wananchi

Aidha Meneja wa mtandao wa Yas  Tanzania Mkoani Manyara Ladislaus Karo amesema kufwatia changamoto ya kijiji cha Gendabi kukumbwa na maporomoko ya matope mwaka 2023  walifanya utafiti nakugundua eneo hilo lina shida ya mtandao nakuona Kuna haja yakuweka mnara kwenye eneo hilo.

Sauti ya Meneja wa mtandao wa Yas  Tanzania Mkoani Manyara Ladislaus Karo

Nao wananchi wa kijiji hicho wameishukuru Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Yas Tanzania kwakuwaletea mnara huo ambao utatoa huduma za internet na kuwasiliana baina ya wananchi hao na maeneo mengine.

Sauti ya baadhi ya wananchi wa kijiji cha Gendabi

Uzinduzi wa mnara huo ni muendelezo wa miradi ya kampuni hiyo ambayo imewekeza zaidi ya  sh Trillion 1kwenye huduma za mawasiliano hapa nchini Tanzania na kuwa kampuni yenye minara zaidi ya elfu 4800 mpaka sasa.