FM Manyara
FM Manyara
5 May 2026, 7:14 pm

Wawekezaji mkoani Manyara wametakiwa kuchangamkia fursa ya kuwekeza biashara mbalimbali ili kujiinua kiuchumi baada ya Geti la Mamire kufunguliwa kwa ajili ya kupitisha magari ya watalii.
Na Mzidalfa Zaid
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga ameyasema hayo leo wakati akiongea katika kikao cha kamati ya uwekezaji mkoa wa Manyara , amesema serikali imefanikisha kufungua geti hilo, hivyo kunapofunguliwa biashara mbalimbali itasaidia wawekezaji kupata huduma muhimu na kukuza uchumi wa mkoa wa Manyara.
Kwa upande wake afisa biashara mkoa wa Manyara Ally Mokiwa ,amesema mkoa wa Manyara una jumla ya wawekezaji 138 ambapo jitihada mbalimbali zinaendelea za kuweka mazingira bora na kuvutia uwekezaji.

Akiwasilisha ripoti ya tiseza , Katibu wa kamati ya uwekezaji mkoa ambae pia ni kamanda wa uhamiaji mkoa Philon Phabian Kyetema amesema kiwango Cha miradi ya upanuzi kinazidi kuongezeka katika mkoa wa Manyara.
