FM Manyara

TAKUKURU  Manyara yawataka wananchi kusherehekea  sikukuu kwa kukataa rushwa

12 December 2025, 7:49 pm

Sauti ya mkuu wa TAKUKURU  mkoa wa Manyara Bahati Haule

Wakati wananchi wakiwa katika  maandalizi ya sikuu za mwisho wa mwaka , Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Manyara, imewataka wananchi mkoani humo kuadhimisha sikukuu hizo kwa kukataa Rushwa.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa leo na mkuu wa TAKUKURU  mkoa wa Manyara Bahati Haule, wakati akiongea na Fm Manyara, amesema kila mwananchi anapaswa kuwa mstari wa mbele kupinga vitendo vya Rushwa.

Sauti ya mkuu wa TAKUKURU  mkoa wa Manyara Bahati Haule

Aidha, amewataka  wananchi kudumisha utawala bora na utawala wa sheria , kuhifadhi amani, haki na utulivu pamoja na kulinda mali na raslimali za Taifa.