FM Manyara

Deira yaendelea kukuza elimu kwa vitendo

1 August 2026, 11:34 pm

Picha ya baadhi ya wanafunzi wa shule ya Deira wakijifunza kwa vitendo katika hifadhi ya Tarangire

Wanafunzi wa Deira English Medium School wametembelea  hifadhi ya Taifa Tarangire , ambapo wamepata fursa ya kujionea vivutio mbalimbali vya utalii na kujifunza kwa vitendo kuhusu uhifadhi wa wanyamapori na mazingira.

Na Mzidalfa Zaid

Mkurugenzi wa Deira English Medium School, Nada Shauri, amesema ziara hizo ni sehemu muhimu ya mchakato wa kujifunza kwani huwapa wanafunzi maarifa ya vitendo yanayoongeza uelewa wao darasani, huku zikiwajengea moyo wa kuthamini na kulinda rasilimali za asili za nchi.

Picha ya Mkurugenzi wa Deira English Medium School, Nada Shauri,

Kwa upande wake, Mkuu wa shule hiyo, Bosco Godfrey, amesema shule imekuwa na utaratibu wa kuwaandalia wanafunzi ziara za kielimu katika hifadhi mbalimbali ili kuwawezesha kujifunza kwa vitendo, kukuza uwezo wa kufikiri kwa kina na kupanua upeo wao wa maarifa nje ya mazingira ya darasani.

Sauti ya Mkuu wa shule hiyo, Bosco Godfrey,
Picha ya Mkuu wa shule hiyo, Bosco Godfrey,

Baadhi ya wanafunzi walioshiriki katika ziara hiyo wamesema wamefurahia kushuhudia kwa karibu wanyamapori na vivutio vingine vya asili walivyokuwa wakivisoma darasani. 

Wameushukuru uongozi wa shule kwa kuendelea kuwaandalia ziara zinazowapa uzoefu halisi wa kujifunza na kuwajengea ari ya kutunza mazingira na maliasili.

Sauti ya baadhi ya wanafunzi wa Deira

Ziara hiyo ni sehemu ya dhamira ya Deira English Medium School ya kutoa elimu bora inayochanganya nadharia na vitendo, hatua inayochangia kuwajenga wanafunzi wenye maarifa mapana, ubunifu na uzalendo katika kulinda urithi wa taifa.

Baadhi ya wanafunzi wa Deira wakiwa ndani ya hifadhi ya Tarangire