FM Manyara

Watatu wadakwa Manyara kwa kujiunganishia umeme kinyemela

7 September 2026, 7:32 pm

Picha ya baadhi ya watumishi wa TANESCO nyumbani kwa mtuhumiwa aliyejiunganishia umeme

Shirika la umeme Tanzania TANESCO mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na jeshi la polisi limewakamata watu watatu wa kitongoji Cha Ndoroboni kijiji cha Kiru six kwa tuhuma za kuunganishiwa umeme kinyume na Sheria .

Na Mzidalfa Zaid

Afisa uhusiano TANESCO mkoa wa Manyara Samwel Mandar amesema TANESCO inaendelea na msako wa kukagua miundombinu ya shirika ikiwemo kukagua mita nakubaini kama kuna wananchi wamejiunganishia umeme kinyume cha sgeria, ambapo amesema watuhumiwa hao wameweka mita feki ambazo hazionyesh i matumizi ya umeme.

Sauti ya Afisa uhusiano TANESCO mkoa wa Manyara Samwel Mandar

Msimamizi wa kitengo Cha udhibiti mapato TANESCO mkoa wa Manyara Maisha Mchuruza amesema watu hao wameunganishiwa umeme bila kufuata utaratibu wa Tanesco na kuwaonya wananchi kuacha tabia hiyo mara moja.

sauti ya Msimamizi wa kitengo Cha udhibiti mapato TANESCO mkoa wa Manyara Maisha Mchuruza

Baadhi ya watuhumiwa ambao wameunganishiwa umeme wamesema waliunganishiwa na mtu Mmoja ambae alijifanya mfanyakazi wa Tanesco na kuwaambia watoe pesa ili waunganishiwe umeme.

Sauti ya Baadhi ya watuhumiwa
Picha ya baadhi ya watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi

Mwenyekiti wa kitongoji cha ndoroboni kijiji cha Kiru six  Ramadhani Juma amesema hana taarifa za wananchi hao kuunganshiwa umeme, ambapo amewataka wananchi wake kufuata hatua zote za kuunganishiwa umeme.

Sauti ya Mwenyekiti wa kitongoji cha ndoroboni kijiji cha Kiru six  Ramadhani Juma
Picha ya baadhi ya miundombinu ambayo wananchi wamejiunganishia umeme.