FM Manyara

Idara ya afya Manyara kukabiliana na magonjwa ya mlipuko

15 September 2026, 12:54 pm

Picha ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method(Picha na Mzidalfa Zaid)

Mkoa wa Manyara kupitia idara ya afya imechukua tahadhari za kukabiliana na magonjwa ya mlipuko yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua za elinino

Na Mzidalfa Zaid

Kufuatia utabiri wa mvua za El Niño katika maeneo mbalimbali nchini, Idara ya Afya mkoani Manyara imechukua tahadhari za kukabiliana na magonjwa ya mlipuko yanayoweza kujitokeza kutokana na mafuriko.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method, amesema tayari wameunda kamati maalumu ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ili kuhakikisha mkoa unakuwa tayari kukabiliana na changamoto zitakazoweza kujitokeza.

Dkt. Method amewataka wananchi kuchukua tahadhari kwa kuzingatia kanuni za afya, ikiwemo kunywa maji yaliyochemshwa na kunawa mikono mara kwa mara, huku akisema idara hiyo inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga na magonjwa ya mlipuko.

Sauti ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method

Kwa upande wake afisa afya Kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Suten Mwabulambo amezungumzia team ambayo ipo tayari iwapo kutatokea changamoto yoyote inayohusiana na mvua zinazotarajiwa kuanza kati ya mwishoni mwa September na mwanzoni mwa October mwaka huu.

sauti ya afisa afya Kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Suten Mwabulambo
picha ya afisa afya Kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Suten Mwabulambo(Picha na Mzidalfa Zaid)