FM Manyara
FM Manyara
24 June 2026, 1:16 am

Mkuu wa mkoa wa Manyara,Queen Sendigaamezindua gari la halmashauri ya wilaya ya Simanjro lenye thamani ya shilingi milioni 180, litakalotumika kwenye shughuli mbalimbali za kuwahudumia wananchi wa wilaya hiyo.
Sendiga amezindua gari hilo leo alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa miradi mbali mbali itakayotembelewa na kugaguliwa na mwenge wa uhuru kwa mwaka 2026 akisema gari hilo litasaidia shughuli zinazofanywa na watumishi wa wilaya hiyo ya simanjiro pamoja na kuwahudumia wananchi.
Aidha, Sendigaameipongeza halmashauri ya wilaya Simanjiro kwa kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo.
