FM Manyara
FM Manyara
14 July 2026, 11:38 pm

Zaidi ya wananchi 5,000 kutoka vijiji vitatu 3 vilivyopo wilayani Babati mkoani Manyara, wamenufaika na mradi wa maji wa Endamaghay uliolenga kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama uliogharimu shilingi Bilion 1.9
Na Emmy Peter
Mradi huo umezinduliwa na Kiongozi wa Mabio za Mwenge wa uhuru kitaifa Wazo Michael Mwang’onda ambapo amesema utekelezaji wa mradi huo unaunga mkono juhudi za serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassani za kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji na kupunguza adha ya kubeba maji kichwani, hususan kwa wanawake na watoto.
Akitoa taarifa ya mradi huo, Meneja wa RUWASA Mkoa wa Manyara, James Kionaomela, amesema mradi huo unahusisha tanki la kuhifadhi maji lenye uwezo wa kubeba lita 100,000 na utawawezesha wananchi kuunganishiwa huduma ya maji moja kwa moja majumbani, hatua itakayorahisisha upatikanaji wa maji kwa jamii.
Aidha,baadhi ya wananchi walionufaika na mradi huo wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa utekelezaji wake, nakusema mradi huo wa maji utawasaidia kuepuka kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya maji pamoja na kuongeza fursa za kufanya shughuli za maendeleo .
