FM Manyara
FM Manyara
15 July 2026, 10:56 pm

Mwenge wa uhuru umekagua na kuweka jiwe la msingi katika daraja la Sigino – Komoto linalounganisha kata ya sigino na kata ya Komoto halmashauri ya mji wa Babati mkoani Manyara
Na Benny Akaro
Mradi huo unaotekelezwa chini ya wakala wa barabara mijini na vijijini TARURA Umegharimu kiasi cha shilingi milioni 900.4
Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Ndg. Wazo Michael Mwang’onda amesema mwenge wa uhuru umefurahishwa na utekelezaji wa mradi huo akiwataka wananchi kuulinda na kuutunza ili uweze kuleta kudumu
Amesema Serikali inaendelea kuboresha na kuwekeza katika miundombinu ya barabara kwa lengo la kuchochea shughuli za kiuchumi na kimaendeleo.
Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo Meneja wa Tarura wilaya ya Babati, Eng. Aloyce Nombo amesema mradi huo ulikadiriwa kukamilika Mei 2026 lakini kutokana na changamoto za hali ya hewa kwasasa unatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika mwezi agosti mwaka huu.
Kwa Upande wake Mbunge wa Jimbo la Babati mjini Mh. Emanuel Khambay ameishukuru Serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi huo ambao uko mbioni kukamilika.
Naye, Naibu waziri wa OR-Utumishi & Utawala Bora Bi.Regina Ndege amesema daraja hilo ni fursa kiuchumi wa wananchi wa pande zote mbili kwa kuwa linaenda kupunguza adha ya kusafiri umbali mrefu kupata huduma na kuuza na kununua bidhaa.
Mradi huo ni miongoni mwa miradi saba yenye thamani ya shilingi Bilioni 8.09 iliyopitiwa na mwenfe wa uhuru 2026 katika halmashauri ya mji wa Babati.
Kauli Mbiu ya Mwenge wa Uhuru 2026 *Amani, Umoja na Mshikamano wa Kitaifa*