FM Manyara

Maafisa  mipango miji  fuatilieni eneo la ujenzi kabla ya  kutoa vibali-RC Sendiga

14 May 2026, 5:22 pm

Picha ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sediga

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga  ametoa maagizo  kwa wataalam wa  mipango miji  mkoani Manyara kuhakikisha wanafatilia  eneo la ujenzi  kwa wananchi  kabla hawajatoa kibali  cha ujenzi.

Na Mzidalfa Zaid

Sendiga amesema hayo  katika kikao cha Baraza la madiwani halmashauri ya mji wa Babati baada ya kubaini uwepo wa ujenzi  holela  katika eneo la daraja la Mrara kwa kukiuka taratibu  za mazingira kutokana na kutofika mita60 kutoka eneo la mto .

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Aidha, amesema mji wa Babati  unakua kwa kasi kiuchumi,na majengo yanapaswa yajengwe kwa utaratibu, ambapo amewaonya maafisa mipango mji  wanaotoa vibali  hivyo bila kufika  eneo husika.