FM Manyara
FM Manyara
22 April 2026, 5:47 pm

Wiki ya nishati ikiwa naendelea kuadhimishwa katika maeneo mbalimbai nchini, shirika la umemee tanzania tanesco mkoa wa manyara limeindelea na ugawaji wa majiko ya nishati safi ya umeme katika maeneo mbali mbali ya mji wa babati.
Na Emmy Peter
Afisa uhusiano Tanesco mkoa wa wa Manyara Samuel Mandari amesema zoezi hilo linaendelea mkoani Manyara ambapo ni juhudi za kuunga mkono serikali katika matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi.
Aidha amesema majiko hayo yanafaida kwa watumiaji na inaokoa garama kwa mwananchi ambapo amesema malipo hayo ni nafuu na utalipa kupitia mita ya umeme unayo tumia.
Sambamba na hayo amesema lengo la ugawaji wa majiko hayo yanayotumia umeme ni kuwasaidia wananchi kupika kwa urahisi na haraka ambapo amewataka mama lishe kutumia nishati hiyo katika biasharaa zao .
Kauli mbiu ya nishati safi katika mkoa wa Manyara ni pika kijanjaa pika na umemee .