FM Manyara

Mamire yasisitiza bajeti jumuishi

4 June 2026, 4:21 pm

Picha ya wanakikundi cha taarifa na maarifa kata ya Mamire

Wanakikundi cha taarifa na maarifa kutoka kata ya Mamire Wilayani Babati Mkoani Manyara wamezipongeza wizara za Afya, Elimu na maji kwa kuweka kipaumbele mrengo wa jinsia  kwenye bajeti zao ambazo zilishawasilishwa kwenye Bunge la 13 linaloendelea huko Jijini Dodoma. 

Na Marino Kawishe

Akihitimisha majadiliano ya siku mbili ya wana KC Mamire, mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa Mkoani Manyara Clara Malley amesema bado Kuna baadhi ya wizara hazionyeshi moja kwa moja namna zitakavyoweka kipaumbele kwenye Bajeti ambazo vinamrengo wa kijinsia. 

Sauti ya mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa Mkoani Manyara Clara Malley

Aidha kwa upande wa baadhi ya wanakikundi waliozungumza na muandishi wa habari wamesema pongezi zao zinaenda moja kwa moja kwenye wizara zilizoonesha kuthamini kile wanachokipambania kwa muda mrefu kutokana na maazimio wanayoweka kwenye vikao vyao vinavyojadili masuala ya Jinsia. 

sauti ya wanakikundi
picha ya wanakikundi wakiendelea na majadiliano ya Bajeti