FM Manyara

Takukuru Manyara yawafunda wadau wa usimamizi wa miradi ya maendeleo

1 July 2026, 12:54 am

Picha ya mkuu wa Takukuru Mkoa wa Manyara Bahati Haule

Na Emmy Peter

Wadau wa usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Manyara wamehimizwa kusimamia ipasavyo utekelezaji wa miradi hiyo ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati, na ubora unaotakiwa ili kuwanufaisha wananchi.

Maelekezo hayo yametolewa leo na mkuu wa wilaya ya Hanang  Halmish Hazal  aliyemuwakilisha mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga katika warsha ya wadau wa usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyoandaliwa na Tasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Manyara iliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa  Manyara.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Hanang’

Awali akizungumza katika warsha hiyo  mkuu wa Takukuru Mkoa wa Manyara Bahati Haule amesema lengo la warsha hiyo  ni kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kuzingatia uwajibikaji, matumizi sahihi ya rasilimali za umma na kuzuia vitendo vya rushwa vinavyoweza kukwamisha utekelezaji wa miradi.

Sauti ya mkuu wa Takukuru Mkoa wa Manyara