FM Manyara

Jamii yatakiwa kuthamini maziwa ya Mama kwa mtoto.

31 July 2026, 7:37 pm

Picha ya Afisa lishe wa halmashauri ya mji wa babati Laurencia Urio (upande wa kulia) akiwa pamoja na Muguzi wa Hospitali ya Mji wa Babati

Ikiwa Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji duniani  yanaanza kesho Agasti mosi jamii Wilayani Babati mkoani Manyara  imehaswa  kuzingatia umuhimu wa maziwa ya mama kwa mtoto  kwa kutambua umuhimu wa kumnyonyesha mtoto pindi anapozaliwa kwa wakati na  ulio sahihi .

Na George Augustino

Hayo yamesemwa leo na Afisa lishe kutoka Halmashauri ya Mji wa Babati Laurencia Urio alipozungumza na Fm Manyara, amesema lengo la uanzishwaji ya wiki ya unyonyeshaji duniani ni kuhamasisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa watoto ili kuimarisha afya za watoto.

Sauti ya Afisa lishe kutoka Halmashauri ya Mji wa Babati

Kwa upande wake Muuguzi kutoka Hospitali ya Mji wa Babati Restituta amesema uimarishaji wa unyonyeshaji unaanzia wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua ambapo mama anatakiwa kuwa na afya njema kwa kuzingatia kula vyakula vyote vyenye virutubisho muhimu ili maziwa yaweze kutoka kwa wingi.

Sauti ya Muuguzi kutoka Hospitali ya Mji wa Babati

Kauli mbiu ya wiki ya unyonyeshaji kitaifa ni “Mwanzo imara wa maisha ya Mtoto, huanza na maziwa ya Mama