FM Manyara
FM Manyara
15 September 2026, 8:53 am

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari za mvua za elinino ambazo zimetabiriwa kunyesha hivi karibuni.
Na Mzidalfa Zaid
Mamalaka ya hali ya hewa Tanzania(TMA) mkoa wa Manyara imeendelea kutoa tahadhari kwa wafugaji,wakulima, wavuvi na wananchi kwa ujumla kufuatia kuwepo kwa mvua za elinino zinazotarajiwa kuanzia wiki ya kwanza mwezi wa Kumi mwaka huu.
Wito huo umetolewa na meneja wa TMA mkoa wa Manyara Salma amour , amesema mvua hizo za elinino zitaleta madhara mbalimbali ikiwemo mafuriko na magonjwa hivyo Wananchi wanapaswa kuchukua hatua za haraka za tahadhari.
Kwa upande wake afisa mwangazi wa hali ya hewa mkoa wa Manyara Haji Hamimu amewataka wananchi kuendelea kufuatilia taarifa za hali ya hewa za Kila siku ili kujua mwenendo wa hali ya hewa.