FM Manyara
FM Manyara
25 May 2026, 4:51 pm

Kaimu mkuu wa wilaya ya Babati ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Kiteto Remidius Mwema , amewataka viongozi wa jeshi la zima moto na uokoaji wilayani Babati mkoani Manyara kutoa elimu kwa wananchi namna ya kukabiliana na majanga kwa kutumia vifaa vya kuzimia moto.
Na Mzidalfa Zaid
Mwema amesema hayo leo alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi vitendea kazi kwa jeshi la zima moto na uokoaji yakiwemo magari,mitambo na boti, ambapo amesema wananchi wengi hawajui namna ya kutumia vifaa vya kuzimia moto ambapo amewataka viongozi hao wa jeshi la zima moto kutoa elimu kwa jamii namna ya kutumia vizimia moto.

Kwa upande wake mkuu wa jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Babati Emmanuel Kibona amesema vitendea kazi hivyo vina thamani ya shilingi billioni 2.4 ambapo amesema vifaa hivyo vitasaidia kurahisisha kazi ya uokoaji kwa wakati .