FM Manyara
FM Manyara
7 June 2026, 3:55 pm

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani (RTO) Mkoa wa Manyara Michael Mwakasungula ameongoza zoezi la ukaguzi wa magari yanayosafirisha watoto katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha usalama wa watoto wakati wa kipindi hiki cha likizo .
Na Emmy Peter
Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mwakasungula amesema lengo la ukaguzi huo ni kuhakikisha watoto wanaosafiri katika kipindi cha shule wanakuwa salama na kufika katika shule bila kupata madhara yanayoweza kuepukika kwa ubovu wa vyombo vya Moto.
Kwa upande wao, baadhi ya madereva WA shule wameeleza kuwa ukaguzi huo ni muhimu kwani unasaidia kuongeza usalama na kuwakumbusha wajibu wao wa kulinda maisha ya watumiaji wa barabara na Watoto kwa ujumla.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara limeendelea kusisitiza ushirikiano wa wananchi na wadau wa usafiri ili kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua na usalama unaimarika katika kipindi chote cha likizo za shule.