FM Manyara

Vikundi vya taarifa na maarifa vyachambua bajeti za wizara ya 2026/2027

28 May 2026, 9:11 pm

Picha ya Mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa Mkoani Manyara Clara Malle akizungumza na wanakikundi wa kituo cha kata yaMamire wilayani babati.

Wakati Bunge la 13 likiendelea  Jijini  Dodoma na Wizara mbali mbali zikiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2026-2027 vituo vya taarifa na maarifa Mkoani Manyara vimepata wasaa wakujadili bajeti za Wizara ya Afya, Elimu, Maji na Kilimo ambazo zilishawasilisha bajeti zao.

Na mwandishi wetu

Akizungumza mbele ya Wanakikundi cha taarifa na maarifa cha Mamire Mratibu wa vikundi hivyo mkoani Manyara Clara Malley amesema lengo la Majadiliano hayo nikutoa maoni ya pamoja ambayo yatafanyiwa kazi na mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP kuona iwapo bajeti hizo zimelenga mrengo wa Jinsia.

Sauti ya Mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa mkoani Manyara Clara Malley
Picha ya wanakikundi wa kata ya mamire

Nao badhi ya wanakikundi cha taarifa na maarifa kutoka kata ya Mamire wamesema walifwatilia Bajeti hizo na kuona zinakidhi takwa lao japo Kuna baadhi ya wizara ikiwemo Wizara ya kilimo haijabainisha moja kwa moja kipaumbele kwenye kilimo cha asili ambacho kinatajwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania kama kilimo chenye Tina kwa vituo hivyo.

Sauti ya wanakikundi

Vituo hivyo vya taarifa na maarifa kutoka mkoani Manyara vinajumuisha kituo cha Mamire kilichopo Kata ya Mamire Wilayani Babati na Murray kilichopo Kata ya Murray Wilayani Mbulu.