FM Manyara

TGNP yawanoa viongozi Babati kupinga ukatili wa kijinsia

17 August 2026, 10:36 pm

Picha ya viongozi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP pamoja na Washiriki wa mafunzo

Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP umafanya mafunzo ya siku mbili  kwa baadhi ya Viongozi kutoka serikali ngazi ya vijiji na kata na wadau mbali mbali wanaojishughulisha na kutoa msaada kwa wahanga au manusura wa matukio ya ukatili wa kijinsia.

Na Marini Kawishe

Akizungumza na Fm Manyara Mwezeshaji kwenye mafunzo hayo Marcela Lungu amesema malengo ya mafunzo hayo ni kuimarisha uwezo wa jamii katika kuzuia, kutambua, kuripoti, kutoa taarifa na kukabiliana na ukatili wa kijinsia ambao kwa kiwango kikubwa upo kwenye jamii.

Sauti ya Mwezeshaji kwenye mafunzo Marcela Lungu

Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo yaliyoanza leo Agust 17 na kumalizika kesho agust 18 wamesema kupatiwa mafunzo kama hayo yamewaongezea uelewa wakukabiliana na ukatili wa kijinsia  ambao unafanyika kwenye jamii na mazingira tofauti na jamii nyingi

Sauti za washiriki wa mafunzo

Mafunzo hayo yanatarajia kuweka mkakati wa pamoja ili kuondoa vikwazo vya ukatili wa kijinsia  ikiwa ni pamoja na uwajibikaji katika mnyororo wa huduma za ukatili kwa kuandaa mpango kazi wenye kubainisha majukumu na wajibu wa wahusika wenye ushawishi katika jamii pamoja na serikali.